Saturday, December 17, 2011

Muitikio mdogo wa wananchi:Kikwazo kwa miradi ya waitaliano Iringa.

Na John Alex.

Muitikio mdogo wa wananchi wa  wa Iringa  katika shughuli za miradi mbalimbali zinazofanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayoendesha shughuli zake kwa ufadhili wa watu wa Italia ni changamoto kubwa inayoyakabili mashirika hayo.

Hayo yamesemwa mwishoni mwa wiki katika maonyesho ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayofadhiliwa na watu wa Italia waishio Mkoani Iringa yaliyofanyika katika hoteli  ya Wilolesi manispaa Ya Iringa.

Katika maadhimisho hayo ambayo yalikutanisha mashirika matatu  yanayofadhiliwa na waitaliano ambayo ni shirika la C.O.P.E(Coooperation for developing countries),shirika la Call Africa lenye miradi yake wilayani Iringa,na shirika la CUAM ambalo linafanya miradi yake mbalimbali ya afya mkoani Iringa.

Wadau wa miradi hiyo wamebainisha changamoto malimbali zinazowakabili katika  utendaji kazi wao huku wote wakilaumu muitikio mdogo hasa wa wananchi katika shughuli za miradi mbalimbali inayofanywa na mashirika yao.

“Kumekuwa na muitikio mdogo sana wa wananchi katika shughuli zinazofanywa na miradi mbalimbali ya shirika letu  la Call Africa kwa mfano akina mama wamekuwa wakikata tama katika kuwapeleka watoto wao katika vituo vya kulelea watoto kama vile Kipepeo Nutritional  centre  ambavyo ni vya kutwa .Hali hii inawapa wakati mgumu wafadhili na ni changamoto kubwa”, anasema Lucas Marano msemaji wa  Call Africa.

Kwa upande wa shirika la CUAM  linalojihusisha na maswala ya afya msemaji  ambae alifahamika kwa jina moja  la Ricado amesema    kuna changamoto kubwa sana hasa katika upatikanaji wa wataalamu wa kutosha  katika kuendeleza program mbalimbali kaitka maeneo lengwa.

Aidha waitaliano hao wamebainisha changamoto nyingine zinazowakabili kuwa ni ushirikiano duni kutoka serikali kwani serikali imekuwa  ikijisahau katika kutoa ushirikiano wa kutosha hususan katika kuhamasisha shughuli mbalimbali za zinazofanywa na miradi ya mashirika  hayo.

Tumeandaa mabango ya usafi katika program yetu ya USAFI rafiki wa maendeleo ,wenye lengo la  kuweka mji wa Iringa  katika hali ya usafi lakini kwa mara kadhaa tumekuwa tukicheleweshwa na wadau manispaa tunawaomba wasiwe wazungushaji katika suala zima la utekelezaji wa miradi ya maenddeleo anasema msemaji wa  Call Africa Lukas Marano.

Miradi mingine  inayofanywa na mashirika hayo matatu ukiiwemo mradiwa  kilimo MAWAKI na mengine mengineyo wamebainisha changamoto zinazofanana na kutaka wananchi wahamasike ili waweze kujikwamua na umasikini na kunufaika na miradi inayofanywa na mashirika haya.
Lengo la maadhimisho ni kutambulisha miradi ya waitalia wanaoishi Tanzania (wilaya za Iringa na Kilolo)kwa ajli ya watoto yatima ,walemavu,wenye mazingira magumu ,mafunzo kwa akina mama  na vijana,huduma ya afya, kilimo,mifugo,ujasiriamali,na  miango maalumu kuhusu UKIMWI

No comments:

Post a Comment