Na John Alex.
Muitikio mdogo wa wananchi wa wa Iringa katika shughuli za miradi mbalimbali zinazofanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayoendesha shughuli zake kwa ufadhili wa watu wa Italia ni changamoto kubwa inayoyakabili mashirika hayo.
Hayo yamesemwa mwishoni mwa wiki katika maonyesho ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayofadhiliwa na watu wa Italia waishio Mkoani Iringa yaliyofanyika katika hoteli ya Wilolesi manispaa Ya Iringa.
Katika maadhimisho hayo ambayo yalikutanisha mashirika matatu yanayofadhiliwa na waitaliano ambayo ni shirika la C.O.P.E(Coooperation for developing countries),shirika la Call Africa lenye miradi yake wilayani Iringa,na shirika la CUAM ambalo linafanya miradi yake mbalimbali ya afya mkoani Iringa.
Wadau wa miradi hiyo wamebainisha changamoto malimbali zinazowakabili katika utendaji kazi wao huku wote wakilaumu muitikio mdogo hasa wa wananchi katika shughuli za miradi mbalimbali inayofanywa na mashirika yao .
“Kumekuwa na muitikio mdogo sana wa wananchi katika shughuli zinazofanywa na miradi mbalimbali ya shirika letu la Call Africa kwa mfano akina mama wamekuwa wakikata tama katika kuwapeleka watoto wao katika vituo vya kulelea watoto kama vile Kipepeo Nutritional centre ambavyo ni vya kutwa .Hali hii inawapa wakati mgumu wafadhili na ni changamoto kubwa”, anasema Lucas Marano msemaji wa Call Africa.
Kwa upande wa shirika la CUAM linalojihusisha na maswala ya afya msemaji ambae alifahamika kwa jina moja la Ricado amesema kuna changamoto kubwa sana hasa katika upatikanaji wa wataalamu wa kutosha katika kuendeleza program mbalimbali kaitka maeneo lengwa.
Aidha waitaliano hao wamebainisha changamoto nyingine zinazowakabili kuwa ni ushirikiano duni kutoka serikali kwani serikali imekuwa ikijisahau katika kutoa ushirikiano wa kutosha hususan katika kuhamasisha shughuli mbalimbali za zinazofanywa na miradi ya mashirika hayo.
Tumeandaa mabango ya usafi katika program yetu ya USAFI rafiki wa maendeleo ,wenye lengo la kuweka mji wa Iringa katika hali ya usafi lakini kwa mara kadhaa tumekuwa tukicheleweshwa na wadau manispaa tunawaomba wasiwe wazungushaji katika suala zima la utekelezaji wa miradi ya maenddeleo anasema msemaji wa Call Africa Lukas Marano.
Miradi mingine inayofanywa na mashirika hayo matatu ukiiwemo mradiwa kilimo MAWAKI na mengine mengineyo wamebainisha changamoto zinazofanana na kutaka wananchi wahamasike ili waweze kujikwamua na umasikini na kunufaika na miradi inayofanywa na mashirika haya.
Lengo la maadhimisho ni kutambulisha miradi ya waitalia wanaoishi Tanzania (wilaya za Iringa na Kilolo)kwa ajli ya watoto yatima ,walemavu,wenye mazingira magumu ,mafunzo kwa akina mama na vijana,huduma ya afya, kilimo,mifugo,ujasiriamali,na miango maalumu kuhusu UKIMWI
No comments:
Post a Comment