Na;John Alex.
Mwaka jana nilibahatika kutembelea vyuo vikuu vya
Mkwawa, Ruaha na Tumaini niliko sasa, hapa mkoani Iringa kujionea hali ya vyuo
hivyo vinavyotoa elimu ya juu nchini.Sikupita kimya kimya ila nilipata fursa ya
kuongea na baadhi ya wadau wa vyuo hivyo vikuu.
Kikubwa walichokizungumza wadau
hawa ni pamoja na changamoto mbalimbali zinazowakabili kama taasisi, lakini jambo
kubwa walilotilia mkazo ni pamoja na miundombinu haba.Uhaba wa kumbi za
kufanyia mihadhara, uhaba wa mabweni jambo ambalo kiukweli lilikuwa ni tatizo
kubwa mno.Hawakuishia hapo wadau walieleza pia mikakati na mipango mbalimbali
wanayoifanya kukabiliana na changasmoto zao huku wakitoa rai kwa taasisi hata
zisizo za kiserikali kutoa misaada
katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili kama taasisi ya kijamii.
Ilikuwa ni jambo la ajabu sana
lakini kwa hali halisi ya kitanzania hatushangai kwa sababu ndio tulivyo na
ndio uwezo wetu.Kuna baadhi ya wanafunzi wa elimu ya juu hapa mkoania Iringa wamekuwa wakielekezwa kuhudhuria vipindi katika
kumbi za mikutano tena za watu binafsi ambazo hutumika kwa shughuli za harusi
na sherehe kwa ujumla.Tumefanya kumbi za sherehe madarasa ya kufanyia mihadhara
na tunalipa sawa na wanavyolipa wengine!Tutafanyaje na wakati hatujajipanga?
Wengine nao karibu asilimia 55 ya
wanafunzi wanaishi nje ya chuo na huko nako ni dhahama tupu,mara huyu
kaibiwa,mwingine kakabwa, sijasikia waliobakwa huenda wapo lakini wanaona aibu kusema.Ni eneo hili hili
wamelalamika kuwa maktaba iliyopo ni ndogo mno.Sasa mnasomea wapi? “Ahhh!
tunajibana hivyo hivyo kwenye majani kama hivi
tunalala kitabu kinakwenda si unajua mabenchi yenyewe machache”
Ni takribani mwaka mmoja
hivi umepita tangu nifanye dodoso zangu
hizo,sasa nimepita tena hivi karibuni kuchunguza je ni kweli mipango na mikakati niliyoambiwa inatekelezwa
imefikia wapi na inaendeleaje.
Kiukweli sina budi kutumia kalamu
yangu kupongeza jitihada mbalimbali
zinazofanywa na wadau hawa wa vyuo vikuu katika kukabiliana na changamoto za
uhaba wa miundombinu ya majengo.Wanajitahidi sana kwani wananchi wenyewe wanajionea kwa
macho.
Ukienda Chuo kikuu Ruaha mjini
pale utajionea namna ujenzi wa miundombinu unavyoendelea tena kwa kasi katika
maeneo ya chuoni na hii ni katika kuhakikisha wanakabilina na changamoto yao ya
uhaba wa kumbi za kufanyia mihadhara yao.Tutasoma kwenye kumbi za sherehe mpaka
lini kama si kudidimiza hadhi ya elimu na chuo kwa ujumla?
Jengo kubwa la maktaba
linaendelea kupanda kwa kasi Chuo kikuu
cha Mkwawa ili kukabilina na changamoto yetu ile ya kusomea kwenye mabenchi
tena machache kwani wengine wanalala kwenye majani ndo wanasoma.Ni
matumaini yangu kuwa hata mikakati ya ujenzi wa mabweni kwa wanafunzi chuoni
hapo imefikia pazuri tu,hapana shaka.Kwa nini wasifanye jitihada na wakati wamepewa
zamana ya kusimamia na kuiendeleza taasisi?Ni kiongozi yupi asiyependa kusifiwa
kwa kuendeleza taasisi na kuifikisha
pazuri.Ah!basi tu umasikini wetu huu ndio unatuponza.
Huku Tumaini nako mambo si mabaya
kwani na wao wanajipanga kihaswa kukabiliana na tatizo hilo.Huku Tumaini kwa
mujibu wa wanafunzi wenyewe wao wanasema
hawalilii sana kukaa ndani si unajua gharama wengine zinawashinda kwa
hiyo mwaka mmoja ndani inayofwata yote nje !Ukisikia anayelilia kupata nafasi
ya kukaa ndani basi ni mgeni huyo ndo kafika.Jengo la kisasa kabisa ujenzi
unaendelea na kama inshalah panapomajaliwa likikamilika basi tutarajie kusikia
tu bwana jamaa wameanzisha kitivo kipya.Kwani ni nani asiyependa maendeleo?
Hapa nchini kwetu si jambo la
kushangaza sana kusikia taasisi Fulani ya elimu ya juu kulalamikia juu ya
miundombinu chakavu nikimaanisha majengo pamoja na vitendea kazi kama magari na
kadhalika lakini muda muafaka unapofika
sharti lazima tubuni mikakati kabambe ya kukabilinana na matatizo yetu haya ambayo kimsingi sisi ndio
chanzo.Kwani wanaozorotesha maendeleo si ni sisi wenyewe haswa pale
tunaponyweshwa pombe na kupewa fulana na kofia halafu tunawachagua kwa hiari
yetu kisha wakiharibu tunalalamika.
Sisi kama watanzania ni lazima
tuhakikishe tunachukua hatua mbadala
hususan katika kuwachagua madereva wetu ambao tunaamini watatufikisha
mahala sisi turidhike na kile wanachokifanya na hivyo tusijutie uamuzi wetu kama tunavyojuta baadhi yetu.Ni uamuzi huu pekee ndio
utazifanya hata taasisi zetu za elimu ya juu zipige hatua katika kufikia
malengo yake.
Sasa miundombinu ya kisasa katika
vyuo vyetu hapa Iringa na nchi nzima kwa ujumla ni miongoni mwa mambo mazuri
ambayo yanatarajiwa yangepewa kipaumbele sana
kiasi ambacho kama ingefanyika hivyo basi
tusingefika mahala tunalalamika oohh!
miundomibnu chakavu mara Gari la wagonjwa hakuna, hivi unafahamu kuwa yote
hutegemea uongozi mzuri?
“Mbona vyuo vingine vinatoza ada
kubwa halafu watu mmekaa kaa kimya tu kama wadudu fulani hivi!Tujiulize kwa
makini je kodi wanayotozwa kama isingekuwepo sidhani kama serikali ingevumilia
kitendo cha watu kupandisha ada kiholela.Kwa mtazamo wangu jibu ni hili; “Kama
wangetufutia kodi kabisa na tusilipe
hata kidogo basi bila shaka sisi hatupendi dhuluma,tungeshusha ada mpaka
kiwango cha chini kabisa.
Miundombinu imara ikiwemo
madarasa ya kisasa yanatoa fursa kwa wasomi wetu kusoma kwa kujiamini
zaidi,kusoma bila bugudhi yeyote na pia kuondoa kero ile ya kusoma huku watu
wakiwa wamesimama kama ilivyo katika vyuo vyetu vikuu baadhi hapa nchini kama sio hapa hapa kwetu Iringa.
No comments:
Post a Comment