Saturday, January 21, 2012

Biashara zadorora chuoni Tumaini.




Na John Alex.

Baaadhi ya wafanya biashara wa vyakula wenye migahawa na wafanya biashara zingine wanaofanya shughuli zao za biashara maeneo ya chuo kikuu Tumaini  wamesema kuwa  katika msimu huu wa sikukuu   biashara ya vyakula na bidhaaa nyingine  maeneo hayo ya chuoni   imekuwa ngumu kupita kiasi.

Wakizungumza na Kwanza jamii kwa nyakati tofauti  wafanya biashara hao wamesema kuwa,  kufuatia likizo fupi  chuoni hapo wanafunzi ambao ndio wanunuzi wakuu wa vyakula  mahotelini na bidhaa nyingine  wamekwenda majumbani kwao kusherehekea sikukuu ya krismasi hali inayopelekea kudorora kwa biashara na wengine kuthubutu hata kuzifunga kabisa kwa muda.

“Asilimia kubwa ya  wateja wetu ni wanafunzi ambao wamekuwa wakinunua vyakula  mahotelini kwa hiyo wanapoondoka inatulazimu wakati mwengine kufunga kabisa hoteli zetu kwani  wanaobaki ni wachache ambao kati yao wapo wanaojipikia wenyewe” anasema Matata Elias .mmoja wa wafanya biashara mwenye mgahawa maarufu maeneo ya Tumaini ujulikanao kwa jina la Agape.

Aidha wafanyabiashra hao wamesema kuwa  biashara ya vyakula na bidhaa nyingine  maeneo hayo ya Tumaini huwa ni ya msimu ambapo wanafunzi wanapokuwa masomoni  biashara huwa inachanganya na pindi tu wafungapo  chuo  wao hulazimika  kufunga   na hivyo shughuli za biashara  kusimma kwa muda mpaka chuo kitakapofunguliwa.

Wafanya biashara hao wameongeza kuwa ugumu wa biashara chuoni hapo hususan kipindi hiki cha karibuni umechangiwa pia na kupanda kwa gharama za maisha  ambapo  wengi  wa wanafunzi inawalazimu kubana matumizi kwa kujipikia wenyewe.

“Hata hawa wachache waliobaki hawatuungishi vizuri kwa kweli nadhani ni kwa sababu ya uchache wao na wengi kuwa wamekwenda  likizo kwa hiyo  wengi wetu inatulazimu kufunga biashara zetu  kutokana na faida ndogo”anasema Hasani Lumato mmoja wa  wafanya biashra wanaojihusisha na ukaangaji wa chipsi.


Hata hivyo kwa upande wa biahsara nyingine kama vile  biashara za vifaa vya maofisini huwa ni kawaida yao pindi ifikapo muda wa likizo huwalazimu kufunga kabisa biashara zao kwani  wanafunzi na wafanya  kazi ambao ndio wanunuuzi wakuu wa bidhaa zao wanakuwa wamekwenda likizo na ambao wanabaki shughuli za masomo na kiofisi husimama.

Wanafunzi wa chuo cha Tumaini wamefunga likizo ndogo kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya krismas  na  wanatarajia kurejea masomoni mara baada  ya sikukuu kuisha mwezi januari 2012.


No comments:

Post a Comment